Thu Mar 17 2022 09:28:55 GMT+0200 (South Africa Standard Time)
This commit is contained in:
commit
e8ab1a269b
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu. \v 2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu. \v 3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote. \v 5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana. \v 7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye. \v 8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua. \v 11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu, \v 13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli. \v 15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, "Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, "Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa. \v 17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo. \v 18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, "Wewe ni nani?" \v 20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, "Mimi sio Kristo." \v 21 Hivyo wakamuuliza, "kwa hiyo wewe ni nani sasa?" Wewe ni Eliya? Akasema, "Mimi siye." Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu," Hapana."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 22 Kisha wakamwambia, "Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma"? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?" \v 23 Akasema, "Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema, \v 25 "Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 26 Yohana aliwajibu akisema, "Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua. \v 27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake." \v 28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, " Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu! \v 30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, "Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.' \v 31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 32 Yohana alishuhudia, "Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake. \v 33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.' \v 34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili, \v 36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, "Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu. \v 38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, "Mnataka nini?" Wakajibu, "Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?" \v 39 Akawambia, "Njooni na mwone."Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro. \v 41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, "Tumempata Masihi" (ambayo inatafsiriwa Kristo). \v 42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, "Wewe ni Simoni mwana wa Yohana" utaitwa Kefa," (maana yake 'Petro').
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, "Nifuate mimi." \v 44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro. \v 45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 46 Nathanaeli akamwambia, "Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?" Filipo akamwambia, Njoo na uone." \v 47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, "Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!" \v 48 Nathanaeli akamwambia, "Umenifahamuje mimi?" Yesu akajibu na akamwambia, "Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 49 Nathanaeli akajibu, "Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli"! \v 50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya." \v 51 Yesu akasema, "Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko. \v 2 Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 3 Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, "Hawana divai." \v 4 Yesu akajibu, "Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia." \v 5 Mama yake akawambia watumishi, "Chochote atakachowambia fanyeni."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 6 Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu. \v 7 Yesu akawambia, "Ijazeni maji mitungi ya mawe." Wakajaza hadi juu. \v 8 Kisha akawambia wale watumishi, "Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza." Wakafanya kama walivyoagizwa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na \v 10 kumwambia, "Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 11 Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 12 Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 13 Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu. \v 14 Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 15 Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao. \v 16 Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, "Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, "Wivu wa nyumba yako utanila." \v 18 Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?" \v 19 Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 20 Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, "Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?" \v 21 Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake. \v 22 Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 23 Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya. \v 24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote. \v 25 Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Basi kulikuwa na Farisayo ambaye jina lake Nikodemo, mmoja wa wajumbe wa baraza la Wayahudi. \v 2 Mtu huyu alimwendea Bwana Yesu usiku na akamwambia, "Rabi, tunajua ya kuwa u mwalimu kutoka kwa Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kutenda ishara hizi zote Mungu asipokuwa pamoja naye."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 3 Yesu akamjibu, "Amini, amini, mtu hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili." \v 4 Nikodemo akasema," Mtu anawezaje kuzaliwa akiwa mzee? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili na kuzaliwa, je anaweza?"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 5 Yesu akajibu, "Amini, amini mtu sipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu. \v 6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili, na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 7 Usishangae kwa sababu nilikuwambia, 'ni lazima kuzaliwa mara ya pili.' \v 8 Upepo huvuma popote upendapo na sauti yake mwaisikia, lakini hamjui utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo hali ya kila aliyezaliwa na roho.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Nikodemo akajibu, kwa kusema, "Mambo haya yawezekanaje?" \v 10 Yesu akamjibu, "Wewe u mwalimu wa Israeli, hata hauyajui mambo haya? \v 11 Amini, amini, nakuambia, kile tunachokifahamu twakishuhudia kwa kile tulichokiona. Lakini hampokei ushuhuda wetu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 12 Kama nimewambia mambo ya hapa duniani na hamuamini, mtawezaje kuamini kama nikiwambia mambo ya mbinguni? \v 13 Maana hakuna aliyepanda juu kutoka mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka, Mwana wa Adamu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 14 Kama vile Musa alivyomwinua nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu lazima ainuliwe, \v 15 ili kwamba wote watakaomwamini wapate uzima wa milele.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, kwamba akamtoa mwanae wa pekee, ili kwamba mtu yeyote amwaminiye asiangamie bali awe na uzima wa milele. \v 17 Kwa sababu Mungu hakumtuma mwanae duniani ili auhukumu ulimwengu, bali kwamba ulimwengu uokolewe katika yeye. \v 18 Amwaminiye Yeye hatahukumiwa. Yeye asiyemwamini tayari ameshahukumiwa kwa sababu hajaliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 19 Hii ndiyo sababu ya hukumu, ya kwamba nuru imekuja ulimwenguni, lakini wanadamu wakapenda giza zaidi ya nuru kwa sababu matendo yao yalikuwa maovu. \v 20 kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru wala haji nuruni ili matendo yake yasije yakawekwa wazi. \v 21 Lakini, yeye atendaye kweli huja kwenye nuru ili matendo yake yaonekane kwamba yametendwa kwa utiifu wa Mungu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 22 Baada ya haya, Yesu pamoja na wanafunzi walienda katika nchi ya Yudea. Huko alitumia muda pamoja nao na alikuwa akibatiza. \v 23 Sasa Yohana pia alikuwa akibatiza huko Ainea karibu na Salim maana kulikuwa na maji mengi pale. Watu walikuwa wakija kwake na kubatizwa, \v 24 kwa kuwa Yohana alikuwa hajatupwa gerezani.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 25 Kisha palitokea mabishano kati ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi kuhusu sikukuuu za utakaso. \v 26 Wakaenda kwa Yohana wakamwambia, "Rabi, yeye uliyekuwa naye ng'ambo ya Mto Yorodani, yeye uliyeshuhudia habari zake, tazama, anabatiza na wote wanaenda wanamfuata."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 27 Yohana akajibu mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa kama amepewa kutoka mbinguni. \v 28 Ninyi wenyewe mwashuhudia kuwa nalisema kuwa, 'mimi sio Kristo', badala yake nilisema, 'nimetumwa mbele yake.'
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 29 Yeye aliye na bibi arusi ni bwana harusi. Sasa rafiki wa bwana arusi, asimamaye na kusikiliza hufurahia sana kwa sababu ya sauti ya bwana arusi. Hii sasa ni furaha yangu iliyotimilika. \v 30 Anapaswa kuzidi, nami napaswa kupungua.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 31 Yeye atokaye juu, yu juu ya yote. Yeye aliye wa ulimwengu anatoka ulimwenguni na huongea mambo ya ki ulimwengu. Yeye atokaye mbinguni yuko juu ya yote. \v 32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna apokeaye ushuhuda wake. \v 33 Yeye aliye pokea ushuhuda wake amehakikisha kuwa Mungu ni mkweli.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 34 Kwa sababu yeye aliyetumwa na Mungu huongea maneno ya Mungu. Kwa kuwa hampi Roho kwa kipimo. \v 35 Baba humpenda Mwana na amempa vitu vyote mikononi mwake. \v 36 Yeye amwaminiye Mwana anao uzima wa milele, lakini kwa yeye asiye mtii Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu hushikamana juu yake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Basi Yesu alipofahamu kuwa Mafarisayo wamesikia kuwa Yesu alikuwa anafuasa na kuwabatiza zaidi ya Yohana, \v 2 (ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake), \v 3 alitoka Judea na akaenda Galilaya.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 4 Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria. \v 5 Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 6 Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana. \v 7 Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, "Nipe maji ninywe." \v 8 Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Yule mwanamke akamwambia, "Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?" Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria. \v 10 Yesu akamjibu, "Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji, ' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 11 Mwanamke akajibu, "Bwana hauna ndoo ya kuchotea, na kisima ni kirefu. Utayapata wapi Maji ya Uzima.? \v 12 Je wewe ni mkuu, kuliko baba yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki, na yeye mwenyewe na watoto wake pamoja na mifugo yake wakanywa maji ya kisima hiki?"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 13 Yesu akajibu, "Yeyote anywae maji haya atapata kiu tena, \v 14 lakini yeye atakaye kunywa maji nitakayompa hatapata kiu tena. Badala yake maji nitakayompa yatakuwa chemchemi inayobubujika hata milele."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 15 Yule mwanamke akamwambia, "Bwana, nayaomba maji hayo ili nisipate kiu, na nisihangaike kuja hapa kuchota maji." \v 16 Yesu akamwambia, "Nenda kamwite mumeo, kisha urudi."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 17 Mwanamke akamwambia, "Sina mume." Yesu akajibu, "Umesema vyema, 'Sina mume;' \v 18 kwa maana umekuwa na wanaume watano, na mmoja ambaye unaye sasa sio mume wako. Katika hili umesema kweli!"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 19 Mwanamke akamwambia, "Bwana naona yakuwa wewe ni nabii. \v 20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu. Lakini ninyi mwasema ya kuwa Yerusalemu ndiyo sehemu ambayo watu wanapaswa kuabudu."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 21 Yesu akamjibu, "Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu au Yerusalemu. \v 22 Ninyi watu mwaabudu kile msichokijua, lakini sisi twaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 23 Hatahivyo, wakati unakuja, na sasa upo hapa, wakati waabuduo kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa sababu Baba anawatafuta watu wa namna hiyo kuwa watu wake wanao mwabudu. \v 24 Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu kwa roho na kweli."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 25 Mwanamke akamwambia, "Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote." \v 26 Yesu akamwambia, "Mimi unayesema nami ndiye."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 27 Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, "Unataka nini?" au "Kwa nini unazungumza naye.?"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 28 Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu, \v 29 "Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?" \v 30 Wakatoka mjini wakaja kwake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 31 Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, "Rabi kula chakula." \v 32 lakini yeye aliwambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi." \v 33 Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula,"Je walileta?"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 34 Yesu akawambia, "Chakula changu ni kufanya mapenzi yake yeye aliyenituma na kutimiza kazi yake. \v 35 Je, hamsemi, 'Bado miezi mitano na mavuno yatakuwa tayari?' Ninawambieni tazameni mashamba yalivyo tayari kwa mavuno! \v 36 Yeye avunaye hupokea mishahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili kwamba yeye apandaye naye avunaye wafurahi pamoja.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 37 Kwa kuwa msemo huu ni wa kweli, 'Mmoja apanda na mwingine avuna.' \v 38 Niliwatuma kuvuna ambacho hamkukihangaikia, Wengine wamefanya kazi na ninyi mmeingia katika furaha ya kazi yao."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 39 Wasamaria wengi katika mji ule walimwani kwa sababu ya taarifa ya yule mwanamke aliyekuwa akishuhudia, "Aliyeniambia mambo yote niliyoyafanya." \v 40 Hivyo Wasamaria walipokuja walimsihi akae pamoja nao na akakaa kwao kwa siku mbili.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 41 Na wengi zaidi wakamwamini kwa sababu ya neno lake. \v 42 Wakamwambia yule mwanamke, "Tunaamini sio tu kwa maneno yako, kwa sababu sisi wenyewe tumesikia, na sasa twafahamu kuwa hakika yeye ni mwokozi wa ulimwengu."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 43 Baada ya siku hizo mbili, akaondoka na kuelekea Galilaya. \v 44 Kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ametangaza kuwa nabii hana heshima katika nchi yake mwenyewe. \v 45 Alipokuja kutoka Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha. Walikuwa wameona mambo yote aliyoyafanya Yerusalemu kwenye sikukuu, kwa sababu na wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye sikukuu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 46 Alikuja tena Kana ya Galilaya huko alikoyabadilisha maji kuwa divai. Palikuwa na ofisa ambaye mwana wake alikuwa ni mgonjwa huko Kapernaumu. \v 47 Aliposikia kuwa Yesu alitoka Judea na kwenda Galilaya, alienda kwa Yesu na kumsihi atelemke amponye mwanawe, ambaye alikuwa karibu kufa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 48 Ndipo Yesu akamwambia, "Ninyi msipoona ishara na maajabu hamwezi kuamini. \v 49 Kiongozi akasema, " Bwana shuka chini kabla mwanangu hajafa." \v 50 Yesu akamwambia, "Nenda mwanao ni mzima." Yule mtu akaamini neno alilolisema Yesu na akaenda zake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 51 Alipokuwa akishuka, watumishi wake walimpokea na kumwambia mwana wake alikuwa mzima. \v 52 Hivyo akawauliza ni muda gani alipata nafuu. Wakajibu, "Jana muda wa saa saba homa ilipomwacha."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 53 Ndipo baba yake akatambua kuwa ni muda ule ule Yesu aliosema, "Mwana wako ni mzima." Hivyo yeye na familia yake wakaamini. \v 54 Hii ilikuwa ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipotoka Yudea kwenda Galilaya.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu. \v 2 Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano. \v 3 Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. {Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. "Wakisubiri maji kutibuliwa.") Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji. \v 4 Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 5 Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao. \v 6 Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, "Je unataka kuwa mzima?"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 7 Yule mgonjwa akamjibu, "Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia." \v 8 Yesu akamwambia, "Inuka na uchukue godoro lako na uende."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 10 Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, "Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako." \v 11 Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, "Chukua godoro lako na uende."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 12 Wakauliza, "Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?''' \v 13 Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 14 Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, "Tazama, umepona! "Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi." \v 15 Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 16 Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato. \v 17 Yesu akawambia, "Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi." \v 18 Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 19 Yesu akawajibu, "Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya. \v 20 Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 21 Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye. \v 22 Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote \v 23 ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 25 Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 26 Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe, \v 27 kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 28 Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake \v 29 nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 30 Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma. \v 31 Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli. \v 32 Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 33 Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli. \v 34 Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa. \v 35 Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 36 Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma. \v 37 Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote. \v 38 Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 39 Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na \v 40 hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 41 Sipokei sifa kutoka kwa watu, \v 42 lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 43 Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea. \v 44 Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 45 Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake. \v 46 Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu. \v 47 Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu.?
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Baada ya mambo haya, Yesu alienda pande za Bahari ya Galilaya, pia huitwa Bahari ya Tiberia. \v 2 Mkutano mkubwa ulikuwa ukimfuata kwa sababu waliona ishara alizozifanya kwa waliokuwa wagonjwa. \v 3 Yesu alipanda juu hadi upande wa juu wa mlima na akakaa huko na wanafunzi wake
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 4 (Na Pasaka, Sikukuu ya Wayahudi ilikuwa imekaribia). \v 5 Yesu alipoinua macho yake juu na kuona umati mkubwa unakuja kwake, akamwambia Filipo, "Tutakwenda wapi kununua mikate ili hawa waweze kula"? \v 6 (Lakini Yesu aliyasema haya kwa Filipo kwa kumjaribu kwa kuwa yeye mwenyewe alijua atakachofanya).
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 7 Filipo akamjibu, "Hata mikate ya thamani ya dinari mia mbili isingelitosha hata kila mmoja kupata hata kipande kidogo." \v 8 Andrea, mmoja wa wanafunzi wake ndugu yake Simoni Petro akamwambia \v 9 Yesu, "Kuna mvulana hapa ana mikate mitano na samaki wawili, lakini hii yafaa nini kwa watu wengi namna hii?"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 10 Yesu akawambia, "Waketisheni watu chini" (kulikuwa na nyasi nyingi mahali pale). Hivyo wanaume wapata elfu tano wakakaa chini. \v 11 Kisha Yesu akachukua ile mikate mitano akashukuru akawawagawia wale waliokuwa wamekaa. Vivyo hivyo akawagawia samaki kwa kadiri ya vile wavyohitaji. \v 12 Watu waliposhiba, aliwambia wanafunzi wake, "Vikusanyeni vipande vya mabaki, vilivyobaki ili kwamba kisipotee chochote."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 13 Basi wakakusanya na kujaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri- vipande vilivyosazwa na wale waliokula. \v 14 Kisha watu walipoona ishara hii aliyoifanya walisema, "Kweli huyu ndiye yule nabii ajaye ulimwenguni." \v 15 Yesu alipotambua kuwa walikuwa wanataka kumkamata ili wamfanye kuwa mfalme wao, alijitenga, tena na akaenda mlimani yeye peke yake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 16 Ilipokuwa jioni, wanafunzi wake walishuka kwenda ziwani. \v 17 Wakapanda kwenye mtumbwi na walikuwa wakivuka kuelekea Kapernaumu. (Giza lilikuwa limeingia na Yesu alikuwa bado hajaja kwao). \v 18 Wakati huo upepo mkali ulikuwa ukivuma, na bahari ilikuwa ikendelea kuchafuka.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 19 Tena wanafunzi wake walipokuwa wamepiga makasia kama ishirini na matano au thelathini, wakamwona Yesu akitembea juu ya bahari kuukaribia mtumbwi, na wakaogopa. \v 20 Lakini akawambia, "Ni mimi! Msiogope." \v 21 Tena walikuwa tayari kumbeba kwenye mtumbwi, na mara mtumbwi ulifika kwenye nchi mahali walipokuwa wakienda.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 22 Siku iliyofuata, mkutano uliokuwa umesimama upande wa bahari waliona kuwa hakuna mtumbwi mwingine isipokuwa ule ambayo Yesu na wanafunzi wake walikuwa hawajaupanda lakini wanafunzi wake walikuwa wameenda zao wenyewe. \v 23 (Ingawa, kulikuwa na baadhi ya mitumbwi iliyotoka Tiberia karibu na mahali walipokula mikate baada ya Bwana kutoa shukrani).
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Wakati makutano walipotambua kuwa sio Yesu wala wanafunzi wake walikuwa kule, wao wenyewe walipanda ndani ya mitumbwi wakaenda Kapernaumu wakimtafuta Yesu. \v 25 Baada ya kumpata upande mwingine wa ziwa wakamuuliza, "Rabbi ulikuja lini huku?"
|
Some files were not shown because too many files have changed in this diff Show More
Loading…
Reference in New Issue