sw_tn/rev/16/intro.md

1.3 KiB

Ufunuo 16 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii ni hitimisho la sehemu kubwa ya kitabu cha Ufunuo ambayo inamalizia kipindi cha hasira ya Mungu ama hukumu kubwa inaletwa na Mungu. (Tazama: rc://*/tw/dict/bible/kt/judge)

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 16:5-7

Dhana muhimu katika hii sura

"Mahali patakatifu sana"

Maelezo haya yamefanya wasomi wengine kuamini kwamba hekalu la Wayahudi lilikuwa na mandhari ya mbinguni. (Tazama: [[rc:///tw/dict/bible/kt/heaven]] na [[rc:///ta/man/translate/writing-apocalypticwriting]])

Hukumu za mabakuli saba

Sura hii inafunua hukumu zinazoitwa hukumu za mabakuli saba. Hukumu hizi zimepewa taswira kama zile ambazo zinamwagwa inje kuashiria haraka na ujumla wa hizo hukumu. (Tazama: rc://*/ta/man/translate/figs-metaphor)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Hisia ya sura hii inakusudiwa kumshtua msomaji. Hii isipunguzwe kwenye tafsiri.

Har-Magedoni

Hili ni neno la Kiebrania na linatumika kama jina la mahali. Yohana anatafsiri herufi za neno hili kwa kuziandika kwa herufi za Kigriki. Watafsiri wanashauriwa kulitafsiri kutumia herufi za lugha kusudiwa.

<< | >>