sw_tn/act/04/23.md

814 B

Maelezo ya jumla

Wakinena pamoja, watu walinukuu Zaburi ya Daudi kutoka Agano la Kale.

Maelezo ya jumla

Neno "wao" linamaanisha baadhi ya waumini, lakini si Petro na Yohana.

Walikuja kwa watu wao

Walikwenda kwa waumini wenzao.

kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema

Hii inamaanisha Roho Mtakatifu alisababisha Daudi kunena au kuandika kile Mungu alichosema.

Kwa kinywa cha baba yetu Daudi

Neno "kinywa" linaelezea yale maneno ambayo Daudi aliyasema ama aliyaandika "Kwa maneno ya baba yetu Daudi"

Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?

Hili ni swali lenye jibu linaloelezea maneno yenye ubatili ya kumpinga Mungu.

watu wametafakari mambo yasiyofaa

Watu wanatafakari maneno ya ubatili yaliyo kinyume na Mungu.