sw_tn/1pe/04/intro.md

1.1 KiB

1 Petero 04 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Tafsiri zingine zimetenga mistari ya ushairi mbele zaidi kuelekea kulia kuliko maandishi mengine ili yasomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la kale katika 4:18

Dhana muhimu katika sura hii

Watu wa mataifa wasiomcha Mungu.

Aya hii inatumia neno "Watu wa mataifa" kumaanisha watu wote wasiomcha Mungu na siyo Wayahudi. Haiwajumuishi Watu wa mataifa ambao wameisha kuwa Wakristo. Zambi za tamaa na ulevi na kuabudu sanamu zilikua tabia ya wasiomcha Mungu.

Kifo cha kishahidi

Ni wazi kwamba Petero anawazungumzia Wakristo wengi ambao wanapitia mateso mengi na wanakaribia kufa kwa ajili ya imani yao.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Na iwe" na "Hata mmoja asi" na "Mwache" na "Wacha hao"

Petero anatumia vifungu hivi vya maneno kuwaeleza wasomaji wake anachotaka wafanye. Ni kama maagizo ya kiamri kwa sababu anataka wasomaje wake wayatii. Lakini ni kama anamwambia mtu mmoja anachotaka na watu wengine wanaambiwa cha kufanya.

<< | >>