sw_tn/1pe/01/intro.md

1.3 KiB

1 Petero 01 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Watafsiri wengine wametenga mistari ya ushairi mbele zaidi kuelekea kulia kuliko maandishi mengine ili yasomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la kale katika 1:24-25.

Dhana maalum katika sura hii

Kile Mungu anafunua

Yesu atakaporudi tena, kila mtu ataona jinsi watu wa Mungu walikuwa wawe na imani kwa Yesu. Halafu watu wa Mungu wataona jinsi Mungu amekuwa wa neema kwao na watu wote watamsifu Mungu na watu wake.

Utakatifu

Mungu anataka watu wake wawe watakatifu kwa sababu Mungu ni Mtakatifu. (Tazama: rc://en/tw/dict/bible/kt/holy)

Milele

Petero anawaambia watu kuishi kwa ajili ya vitu vya kudumu milele na kuacha kuishi kwa ajili ya vitu vya dunia hii ambavyo vitaisha. (Tazama: rc://en/tw/dict/bible/kt/eternity)

Maswala mengine ya utata katika sura hii

Ukweli kinza

Ukweli kinza ni kauli ya ukweli ambayo inaonekana kuelezea kitu kisichowezekana. Petero anaandika kwamba wasomaji wake wanafurahi na kuhuzunika kwa wakati mmoja (1 Petero 1:6). Anaweza kusema hivi kwa sababu wanahuzuni kwa sababu wanateseka lakini wanafurahi kwa sababu wanafahamu kwamba Mungu atawaokoa nyakati za mwisho" (1 Peter 1:5)

| >>