sw_tn/rom/09/intro.md

2.3 KiB

Warumi 09 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sura hii, Paulo anaacha mafundisho ya kwanza. Katika Sura ya 9-11, anazingatia taifa la Israeli.

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB hufanya hivi kwa mistari 25-29 na 33 ya sura hii. Paulo ananukuu maneno haya yote kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Mwili

Paulo anatumia neno "mwili" katika sura hii kutaja Waisraeli, wazao wa Abrahamu kupitia Yakobo, ambaye Mungu alimwita Israeli. (See: rc://*/tw/dict/bible/kt/flesh)

Katika sura nyingine, Paulo anatumia neno "ndugu" kumaanisha Wakristo wenzake. Hata hivyo, katika sura hii, anatumia "ndugu zangu" kumaanisha jamaa zake Waisraeli.

Paulo anaelezea wale wanaomwamini Yesu kama "watoto wa Mungu" na "watoto wa ahadi."

Kuchaguliwa mapema

Wasomi wengi wanaamini kama Paulo katika sura hii anafundisha sana juu ya somo inayojulikana kama "kuchaguliwa mapema." Hii inahusiana na dhana ya Biblia ya "kuchagua mapema." Wengine huchukua hii ili kuonyesha kwamba Mungu, tangu kabla ya msingi wa dunia, alichagua watu wengine kuokoa milele. Wakristo wana maoni tofauti juu ya kile Biblia inafundisha juu ya suala hili. Hivyo watafsiri wanahitaji kuchukua tahadhari ya ziada wakati wa kutafsiri sura hii, hasa kuhusiana na mambo ya kusababisha. (See: [[rc:///tw/dict/bible/kt/predestine]] and [[rc:///tw/dict/bible/kt/save]])

Mifano muhimu y matamshi katika sura hii

Jiwe la kikwazo

Paulo anaelezea kwamba ingawa Wayunanai wamoja wamempokea Yesu kama mwokozi wao kwa kumwamini, Wayahudi wengi walikuwa wanajaribu kupata wokovu wao kwa kufanya kazi wenyewe na hivyo wakamkataa Yesu. Paulo, akinukuu Agano la Kale, anaelezea Yesu kama jiwe ambalo Wayahudi wanakumbwa wakati wa kutembea. "Jiwe la kuwakwaza" huwafanya "kuanguka." (See: rc://*/ta/man/translate/figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Sio kila mtu wa Israeli ambaye ni wa Israeli"

Paulo anatumia neno "Israeli" katika aya hii kwa maana mbili tofauti. "Waisraeli" ya kwanza inamaanisha wazao wa Abrahamu kupitia Yakobo. "Waisraeli" ya pili ina maana wale ambao ni watu wa Mungu kupitia imani. UDB inaonyesha hii.

<< | >>