sw_tn/psa/109/028.md

762 B

Ingawa wananilaani

Wanaozungumziwa ni watu wanaomshtaki Daudi na kusema vitu vibaya kumhusu.

na waaibishwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na waaibike" au "acha waaibike"

lakini watumishi wako wafurahi

"lakini mimi, mtumishi wako, nifurahi" au "mimi ni mtumishi wako, acha nifurahi." Daudi anatumia msemo "mtumishi wako" kumaanisha ni yeye.

Na washindani wangu wavikwe ... na wavae

Misemo hii miwili ina maana ya kufanana na inatumika kusisitiza jinsi anavyotamani sana waaibishwe.

wavikwe aibu

Hapa Daudi anawazungumzia kuaibika kana kwamba ilikuwa vazi walilovaa. "waaibike sana"

na wavae aibu yao kama joho

Daudi anawazungumzia kuaibika kana kwamba ilikuwa joho walilovaa. "na aibu yao iwafunike kama joho walilojifunika"