sw_tn/psa/019/013.md

1013 B

Muweke mtumishi wako pia mbali na

Lahaja hii inaonesha mtumishi kama ametolewa kwenye dhambi ambazo hataki kutenda. "Pia, mlinde mtumishi wako kutokufanya" au "Pia, hakikisha sifanya"

mtumishi wako

Daudi anajiita "mtumishi wako" anapozungumza na Mungu kama ishara ya heshima. "mimi"

usiziache zinitawale

Dhambi zinaelezwa kana kwamba ni mfalme anayeweza kutawala juu ya mtu. "usiache dhambi zangu ziwe kama mfalme anayetawala juu yangu"

sina hatia na makosa mengi

"sina hatia ya kuasi dhidi yako" au "sina hatia ya kutenda dhambi nyingi"

maneno ya mdomo wangu na mawazo ya moyo wangu

Misemo hii pamoja inaeleza kile ambacho mtu anasema na kuwaza. "vitu ninavyosema na vitu ninavyowaza"

yakubalike machoni pako

"yapokee kukubaliwa machoni pako" au "yakupendeze wewe"

machoni pako

Hii inamaanisha Mungu mwenyewe. "kwako"

Yahwe, mwamba wangu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni mwamba ambao mtu anaweza kupanda kujilinda dhidi ya adui zake. "Yahwe, wewe ni kama mwamba wangu"