sw_tn/mat/11/intro.md

1.0 KiB

Mathayo 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huingiza kidogo mistari ya nukuu kutoka kwa Agano la Kale. ULB inafanya hivyo kwa mistari ya nukuu zilizotajwa katika 11:10.

Wasomi wengine wanaamini kwamba Mathayo 11:20 huanzisha hatua mpya katika huduma ya Kristo kwa sababu ya kukataliwa kwake na Israeli.

Dhana maalum katika sura hii

Ufunuo uliofichwa

Baada ya Mathayo 11:20, Yesu anaanza kufunua habari kumhusu yeye mwenyewe na kuhusu mipango ya Mungu Baba, huku akificha habari hii kwa wale wanaomkataa. (Angalia: Mathayo 11:25)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ufalme wa mbinguni umekaribia"

Maneno haya yana umuhimu mkubwa wa kitheolojia. Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."

<< | >>