Baada ya Mathayo 11:20, Yesu anaanza kufunua habari kumhusu yeye mwenyewe na kuhusu mipango ya Mungu Baba, huku akificha habari hii kwa wale wanaomkataa. (Angalia: Mathayo 11:25)
Maneno haya yana umuhimu mkubwa wa kitheolojia. Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."