sw_tn/mat/09/12.md

1.1 KiB

Maelezo y a jumla

Matukio haya yanatokea kwenye nyumba ya Mathayo mtoza ushuru.

Na Yesu aliposikia hayo

Hapa "hayo" inarejea swali ambalo mafarisayo waliuliza kuhusu Yesu kula na watoza ushuru na wenye dhambi.

Watu walio na afya nzuri hawahitaji mganga, isipokuwa wale walio wagonjwa

Yesu anajibu kwa kutumia mithali. Anamaanisha kuwa anakula na watu wa aina hii kwa sababu amekuja kuwaokoa wenye dhambi.

watu walio na afy nzuri

"watu wenye afya"

wale walio wagonjwa

Kirai "wanahitaji mganga" kinaeleweka. "Wagonjwa ndio wanaohitaji mganga"

Inawapasa muende mukajifunze maana yake

Yesu anaelekea kunukuu maandiko. "Inakupasa ujifunze maana ya kile ambacho Mungu alisema katika maandiko"

Inawapasa muende

Kiwakilishi "wa" ni cha wingi kinachomaanisha mafarisayo

Ninapenda rehema na wala siyo dhabihu

Yesu ananukuu kile ambacho nabii Hosea aliandika katika maandiko.. Hapa "Ni" inamaanisha Mungu.

Kwa kuwa nilikuja

Hapa "Ni" inamaanisha Yesu.

haki

Yesu anatumia kejeli. Hadhani kuwa kuna watu wenye haki ambao hawahitaji kutubu. "wale wanaodhani kuwa ni wenye haki"