forked from WA-Catalog/sw_tn
40 lines
1.1 KiB
Markdown
40 lines
1.1 KiB
Markdown
|
# Maelezo y a jumla
|
||
|
|
||
|
Matukio haya yanatokea kwenye nyumba ya Mathayo mtoza ushuru.
|
||
|
|
||
|
# Na Yesu aliposikia hayo
|
||
|
|
||
|
Hapa "hayo" inarejea swali ambalo mafarisayo waliuliza kuhusu Yesu kula na watoza ushuru na wenye dhambi.
|
||
|
|
||
|
# Watu walio na afya nzuri hawahitaji mganga, isipokuwa wale walio wagonjwa
|
||
|
|
||
|
Yesu anajibu kwa kutumia mithali. Anamaanisha kuwa anakula na watu wa aina hii kwa sababu amekuja kuwaokoa wenye dhambi.
|
||
|
|
||
|
# watu walio na afy nzuri
|
||
|
|
||
|
"watu wenye afya"
|
||
|
|
||
|
# wale walio wagonjwa
|
||
|
|
||
|
Kirai "wanahitaji mganga" kinaeleweka. "Wagonjwa ndio wanaohitaji mganga"
|
||
|
|
||
|
# Inawapasa muende mukajifunze maana yake
|
||
|
|
||
|
Yesu anaelekea kunukuu maandiko. "Inakupasa ujifunze maana ya kile ambacho Mungu alisema katika maandiko"
|
||
|
|
||
|
# Inawapasa muende
|
||
|
|
||
|
Kiwakilishi "wa" ni cha wingi kinachomaanisha mafarisayo
|
||
|
|
||
|
# Ninapenda rehema na wala siyo dhabihu
|
||
|
|
||
|
Yesu ananukuu kile ambacho nabii Hosea aliandika katika maandiko.. Hapa "Ni" inamaanisha Mungu.
|
||
|
|
||
|
# Kwa kuwa nilikuja
|
||
|
|
||
|
Hapa "Ni" inamaanisha Yesu.
|
||
|
|
||
|
# haki
|
||
|
|
||
|
Yesu anatumia kejeli. Hadhani kuwa kuna watu wenye haki ambao hawahitaji kutubu. "wale wanaodhani kuwa ni wenye haki"
|