sw_tn/mat/03/04.md

745 B

Sasa...asali ya nyikani

Neno "sasa" limetumika hapa kuweka alama kutenganisha mtiririko mkuu wa simulizi. Hapa Mathayo ana simulia habari za historia ya nyuma kuhusu Yohana Mbatizaji.

alivaa nguoa za manyoa ya ngamia na mkanda wa ngozi katika kiuno chake.

Vazi hili huashiria kwamba Yohana ni nabii kama manabii wa tangu zamani, hususan nabii Eliya.

Kisha Yerusalemu, Uyahudi yote, na mkoa wote

Hii humaanisha watu kutoka maeneo yale. "Hapa neno "yote" humaanisha "wengi." Mathayo anasisitiza jinsi watu wengi walivyoenda kwa Yohana Mbatizaji.

Walibatizwa naye

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Yohana aliwabatiza."

Wao

Hii inamaanisha watu waliokuja kutoka Yerusalemu, Uyahudi, na mkoa kuzunguka Mto Yordani.