sw_tn/mat/02/17.md

1.0 KiB

Taarifa kwa ujumla:

Mwandishi amnukuu nabii Yeremia kuonesha kwamba kifo cha watoto wote wa kiume katika mkoa wa Bethlehemu kilikuwa kwa mujibu wa Maandiko.

Kisha ilitimizwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Hii ilitimizwa" au "matendo ya Herode yalitimiza."

kile kilicho kuwa kimenenwa kwa njia ya nabii Yeremia

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kile Bwana alikinena hapo zamani kwa njia ya nabii Yeremia"

Sauti ilisikika...hawakuwapo

Mathayo anamnukuu nabii Yeremia.

Sauti ilisikika

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Watu walisikia sauti" au "kulikuwa na sauti kubwa."

Raheli awalilia watoto wake

Raheli aliishi miaka mingi kabla ya wakati huu. Unabii huu huonesha Raheli, ambaye amekufa, akiwalilia wazaliwa wake.

alikataa kufarijiwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "hakuna yeyote angeweza kumfariji"

kwa sababu hawapo tena

kwa sababu watoto walikuwa wametoweka na kamwe hawatarudi." Hapa "hawapo tena" ni njia laini ya kusema wamekufa. "kwa sababu walikuwa wamekufa"