sw_tn/luk/19/intro.md

2.3 KiB

Luka 19 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Luka 19:11-27 ni mfano mmoja. Mfano huu unawafundisha Waumini jinsi ya kuishi katika Ufalme wa Mungu utakapokuja. Wasikilizaji wa Yesu waliamini kimakosa kwamba ufalme huo ungeonekana haraka sana. Ingawa ufalme unaweza kuonekana wakati wowote, maneno haya hayana maana ya kusema ufalme utatokea leo au kesho, lakini itawezekana. (See: rc://*/tw/dict/bible/kt/kingdomofgod)

Dhana maalum katika sura hii

"Mwenye dhambi"

Mafarisayo hutaja kundi la watu kuwa "wenye dhambi." Viongozi wa Kiyahudi walidhani watu hawa walikuwa wenye dhambi, lakini kwa kweli viongozi wenyewe walikuwa pia wenye dhambi. Hali hii inaweza kuchukuliwa kama kinaya. (See: [[rc:///tw/dict/bible/kt/sin]] and [[rc:///ta/man/translate/figs-irony]])

Usimamizi

Ingawa neno hili haitumiwi katika sura hii, ni neno kubwa katika mafundisho haya. Usimamazi ni kuwa mwaminifu katika vitu umepewa kwa kuchungu. Mungu anatarajia kila mtu kutumia vipaji alivyompa. Hii sio tu vipaji au uwezo ambao Mungu amempa mwanadamu, lakini maisha ya mtu anayoyaishi katika matarajio ya uzima wa milele. Mungu pia anatarajia watu kuishi katika matarajio ya kurudi kwa Yesu.

Mwana-punda

Jinsi ambavyo Yesu aliingia Yerusalemu, akiwa amepanda mnyama, ilikuwa sawa na vile ambavyo mfalme angeingia katika mji baada ya ushindi mkubwa. Na kwa wafalme wa Israeli, ilikuwa desturi kupanda punda badala ya farasi. Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya tukio hili, lakini hawakuandika maelezo sawa. Mathayo aliandika kuhusu kuwepo kwa punda na mwana-punda, lakini haijulikani ni yupi ambaye Yesu alipanda. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kuwafanya wote kusema jambo sawa. (Tazama:Mathayo 21:1-7 na Yohana 12:14-15)

Kutandaza mavazi na matawi

Hii ilikuwa njia ya kumheshimu mfalme.

"[Yesu] akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza"

Imeandikwa kama Yesu alisafisha hekalu kwa kufukuza wafanyabiashara wasio watu wa Mungu kutoka hekaluni. Tukio hili linaonyesha mamlaka ambayo Yesu alikuwa nayo juu ya hekalu na taifa la Israeli. (See: [[rc:///tw/dict/bible/kt/clean]] and [[rc:///tw/dict/bible/kt/ungodly]])

<< | >>