sw_tn/luk/18/intro.md

1.9 KiB

Luka 18 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Luka 18:6-8 inapaswa kuonekana kama maelezo ya mfano katika 18:1-5.

Dhana maalum katika sura hii

Hakimu asiye na haki

Waamuzi walitakiwa kuendesha haki bila masharti, lakini hakimu huyu hamtendei mwanamke haki. Badala yake, anapaswa kuomba mara nyingi kwa hakimu kufanya jambo linalofaa. Kwa hiyo, hakimu alionyeshwa kama 'asiye na haki." (See: [[rc:///tw/dict/bible/kt/justice]] and [[rc:///tw/dict/bible/kt/unjust]])

Mafarisayo na watoza ushuru

Luka mara kwa mara anaonyesha kuwa tofauti makundi haya mawili ya watu katika injili yake. Mafarisayo walijiona kuwa ni mifano ya wazi ya wenye haki na kuona watoza ushuru kuwa wenkye dhambi sana, mifano ya wazi ya uovu. (See: [[rc:///tw/dict/bible/kt/righteous]], [[rc:///tw/dict/bible/kt/unrighteous]] and rc://*/tw/dict/bible/kt/sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

"Aliomba mambo haya juu yake mwenyewe"

Sala ya Mfarisayo kwa hakika haielekezwi kwa Mungu, kwa hiyo kile anachofanya sio maombi. Yeye anadhani anaomba, lakini anazungumza tu ili watu wengine wamsikie na kufikiri kuwa ni mtakatifu.

Maelekezo ya jumla na Maalum

Kuna nyakati ambapo Agano Jipya inatoa maelekezo maalum au amri ambazo zinahusu Wakristo wote. Kwa nyakati nyingine, maelekezo yake ni ya jumla au hata kupita kiasi. Kwa mfano, wakati Yesu anasema, "Uza vitu vyako," hazungumzii na Wakristo wote mahali pote wakati wote, lakini Wakristo wote wanapaswa kukumbuka kwamba wao ni mawakili tu wa kila kitu wanachopokea kutoka kwa Mungu, na anaweza kuwaomba kukitoa wakati wowote. (See: rc://*/ta/man/translate/figs-hyperbole)

<< | >>