sw_tn/jhn/20/intro.md

1.5 KiB

Yohana 20 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Pokea Roho Mtakatifu"

Wanafunzi walikuwa na nguvu maalum waliopewa na Roho Mtakatifu. Aliiwezesha huduma yao.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Raboni

Hii ni neno la Kiebrania. Yohana "alifasiri" sauti zake kwa kubadilisha herufi za Kiebrania na kutumia herufi za Kigiriki. Kisha anaeleza kwamba maana ya neno hili ni Mwalimu." Mtafsiri anatakiwa kufanya hivyo, lakini aifasiri kwa kutumia herufi za lugha inayolengwa.

Mwili wa Yesu wa ufufuo

Kuna siri juu ya mwili wa Yesu wakati huu. Alikuwa kimwili mwenye makovu kutoka kusulubiwa lakini pia aliweza kuingia katika vyumba bila kutumia mlango. Ni vyema kuiacha hii siri mahali pale lakini maelezo yanaweza kuwa muhimu ikiwa tafsiri haieleweki kwa msomaji.

Malaika wawili wenye mavazi meupe

Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya malaika waliovalia nguo nyeupe wakiwa pamoja na wanawake katika kaburi la Yesu. Waandishi wawili kati yao waliwaita wanaume, lakini ni kwa sababu tu malaika walikuwa katika hali ya kibinadamu. Waandishi wawili waliandika kuhusu malaika wawili, lakini waandishi wengine wawili waliandika juu ya moja tu. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kufanya vifungu vyote kufanana.(Angalia: Mathayo 28: 1-2, Marko 16: 5 na Luka 24: 4 na Yohana 20:12)

<< | >>