sw_tn/isa/30/14.md

800 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anafafanua jinsi Yahwe ataangamiza watu wa Yuda.

Ativunja

Hapa "ataivunja" ina maana ya sehemu ya ukuta ambayo inakaribia kuanguka. Sehemu katika ukuta ni sitiari ambayo inawakilisha watu wa Yuda na dhambi yao iliyotajwa katika 30:12

kama chombo cha mfinyanzi kinavyovunjwa

Tashbihi hii ina maana ya kwamba kipande cha ukuta kitavunjika haraka na kikamilifu kama jagi la udongo linapoanguka chini.

mfinyanzi

Mfinyanzi ni mtu ambaye hutengeneza vyungu na majagi kwa udongo.

hakutapatikana

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu ataweza kupata" au "hapatakuwa"

kigae ambacho kitatumika kukwangua

"kigae kikubwa ya kutosha kukwangua"

moto kutoka katika meko

Neno "moto" hapa lina maana ya majivu. "majivu kutoka katika sehemu ya moto"