sw_tn/isa/27/04.md

1.3 KiB

Kauli Kiunganishi

Hii inaendelea kuzungumza kuhusu watu wa Israeli kana kwamba walikuwa shamba la mizabibu.

Sina hasira, Oh, hata kuwe na mibigili na miiba! Katika vita nitatembea dhidi yao

"Sina hasira. Kama kulikuwa na mibigili na miiba ningetembea dhidi yao katika vita"

Sina hasira

Inaeleweka ya kwamba Yahwe hana hasira na watu wake tena. "Sina hasira na watu wangu tena"

hata kuwe na mibigili na miiba

Adui za watu wa Israeli wanazungumziwa kana kwamba walikuwa mibigili na miiba inayoota katika shamba la mizabibu.

mibigili na miiba

Mibigili na miiba hutumika mara kwa mara kama alama ya miji na nchi zilizoharibiwa

Katika vita nitatembea dhidi yao

Yahwe kupigana na adui zake inazungumziwa kana kwamba alikuwa mwanajeshi katika jeshi.

Ningetembea dhidi yao; Ningewachoma wote kwa pamoja

Hapa Isaya anaunganisha picha tofauti kuzungumzia maadui wa Yahwe. Anazungumza juu yao kana kwamba walikuwa mibigili na miiba lakini pia kama wanajeshi katika jeshi.

isipokuwa washike ulinzi wangu

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "ulinzi" ielezwe kama kitenzi "kulinda". "Isipokuwa waniulize kuwalinda wao"

na kufanya amani pamoja na mimi; waache wafanya amani pamoja na mimi

"na waombe kuishi kwa amani pamoja nami; ninataka waishi kwa amani pamoja nami"