sw_tn/isa/01/29.md

554 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Miti ya mwaloni mitakatifu ... bustani

Misemo hii ina maana ya sehemu ambapo watu wa Yuda waliabudu sanamu.

utaaibika kwa

Baadhi ya tafsiri husema, "utaona aibu kwa sababu ya". Mtu huona aibu uso wake unapochemka, mara kwa mara kwa sababu anahisi amefanya kitu kibaya.

Kwa maana utakuwa kama mwaloni ambao majani hufifia, na kama bustani ambayo haina maji

Maji hutoa uhai kwa miti na bustani. Watu wamejikata kutoka kwa Yahwe, ambaye hutoa uhai.