sw_tn/gen/35/16.md

1.0 KiB

Efrathi

Hili ni jina lingine la mji wa Bethelehemu.

akashikwa na uchungu

"Alikuwa na wakati mgumu wakati alipokuwa akimzaa mtoto"

Alipokuwa katika utungu mzito zaidi

"Uchungu ulipokuwa katika hatua mbaya zaidi"

mkunga

mtu anayemsaidia mwanamke anapojifungua mtoto

Hata alipokaribia kufa, kwa pumzi yake ya mwisho

"pumzi yake ya mwisho" ni pumzi ya mwisho ya mtu kabla mtu hajafa. "Hata kabla hajafa, alipovuta pumzi yake ya mwisho"

Benoni

"Jina la Benoni lina maana ya "mtoto wa majonzi yangu""

Benyamini

Watafsiri wanaweza kuweka maandishi mafupi yasemayo "Jina la Benyamini lina maana ya "mtoto wa mkono wa kuume". Msemo wa "mkono wa kulia" unalenga sehemu yenye upendeleo maalumu.

na kuzikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na wakamzika"

katika njia

"pembeni mwa barabara"

ndiyo alama ya kaburi la Raheli hata leo

"inaweka alama juu ya kaburi la Raheli mpaka siku hii"

hata leo

"mpaka wakati huu wa leo." Hii ina maana hadi wakati ambapo mwandishi alikuwa akiandika haya.