sw_tn/gen/15/17.md

969 B

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuwa makini kwa taarifa ya kushangaza inayofuata.

moshi wenye moto na miali ya mwanga ilipita kati ya vile vipande

Mungu alifanya hivi kumuonyesha Abramu ya kuwa alikuwa akifanya agano na yeye.

ilipita kati ya vile vipande

"ilipita katikati ya mistari miwili ya vipande vya wanyama"

agano

Katika agano hili Mungu alimuahidi kumbariki Abramu, naye ataendelea kumbariki ikiwa Abramu ataendelea kumfuata yeye.

Ninatoa nchi hii

Kwa kusema hivi, Mungu alikuwa akiwapa uzao wa Abramu nchi. Mungu alikuwa akifanya hivi, lakini uzao hawakuweza kwenda katika nchi hadi baada ya miaka mingi baadae.

mto mkuu, Frati

"mto mkubwa, Frati". Hizi ni njia mbili zinazoelezea mto mmoja.

Mkeni , Mkenizi, na Mkadmoni, Mhiti, Mperizi, Mrefai, Mwamori, Mkanaani, Mgirgashi, na Myebusi.

Haya ni majina ya makundi ya watu ambao waliishi katika nchi. Mungu angeruhusu uzao wa Abrahamu kuwashinda watu hawa na kuchukua nchi yao.