sw_tn/act/21/22.md

710 B

Taarifa ya jumla

Fungu hili limawahusu Yakobo na wazee wengine.

watu wanne ambao waliweka kiapo

Hii ilikuwa ni aina ya kiapo ambapo mtu hakutaka kunywa kileo au kukata nywele zao mpaka mwisho wa kipindi cha kuweka muda. "watu wanne ambao walitoa ahadi kwa Mungu."

Wachukue watu hawa na ujitakase mwenyewe pamoja nao

Walikuwa wanapaswa wao wenyewe kujitakasa ili waweze kuabudu ndani ya hekalu.

na uwalipie gharama zao

Lipa kile ambacho watahitaji kulipiwa.

ili waweze kunyoa vichwa vyao

Hii ni ishara ya mtu anayetimiza nadhili yake kwa Mungu.

mambo waliyoambiwa kuhusu wewe

Mambo ambayo yanasemwa na watu kukuhusu wewe.

Kufuata sheria

Inamaanisha utii wa kuzishika sheria za Mungu.