sw_tn/act/14/03.md

1.3 KiB

Maelezo ya jumla

Hapa neno "Yeye" linamaanisha Bwana.

Kwa hiyo wakabaki kule

"Hata hivyo walibaki kule." Paul na Barnaba walibaki ikonia kuwasaidia watu wengi walioamini katika 14:1. "Kwa hiyo" inaweza kuondolewa kama itaongeza mchanganyiko kwenye maandishi.

kutoa uthibitisho kuhusu ujumbe wa neema yake

"kuonesha kwamba ujumbe kuhusu neema yake ni kweli"

kuhusu ujumbe wa neema yake

"kuhusu ujumbe wa neema ya Bwana"

kwa kuruhusu ishara na maajabu kufanywa na mikono ya Paulo na Barnaba.

HIi inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa kuwawezesha Paulo na Barnaba kufanya ishara na maajabu"

kwa mikono ya Paulo na Barnaba

Hapa "mikono" inamaanisha nia na juhudi za wanaume hawa wawili kulingana na walivyoongozwa na Roho Mtakatifu. "kwa huduma ya Paulo na Barnaba"

sehemu kubwa ya mji uligawanyika

Hapa "mji" inamaanisha watu waliomo kwenye mji. "watu wengi wa mji waligawanyika" au "watu wengi wa mji hawakukubaliana"

walikuwa upande wa wayahudi

"waliaunga mkono Wayahudi" au "walikubaliana na Wayahudi." Kundi la kwanza lililotajwa halikukubaliana na ujumbe kuhusu neema.

na mitume

Kundi la pili lililotajwa lilikubaliana na ujumbe kuhusu neema. Inaweza kusaidia kutaja tena kitezi. "walijiunga na mitume"

mitume

Luka anamaanisha Paulo na Barnaba. Hapa "mitume" inaweza kutumika katika hali ya ujumla ya "wale waliotumwa nje."