sw_tn/act/02/40.md

704 B

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya habari kwa tukio la siku ya Pentekoste. Inaanza sehemu nyingine inayoelezea jinsi gani waumini waliendelea kuishi baada ya siku ya Pentekoste.

alishuhudia na kuwasihi

"Aliwaambia waziwazi na kuwasihi waitikie kwa ujumbe alioutoa kwao.

Jiokoeni mtoke katika kizazi hiki kiovu

Wajiokoe kutoka katika adhabu ya Mungu itakayowapata watu waovu.

wakayapokea maneno yake

Inamaanisha wakayapokea maneno aliyoyasema Petro kuwa yalikuwa ya kweli.

Walibatizwa

Wote walioamini walibatizwa.

hapo wakaongezeka katika siku hiyo kama watu elfu tatu

"watu wapatao elfu tatu waliongezeka"

katika kuumega mkate

Walishiriki na kula chakula kwa pamoja