sw_tn/1jn/03/16.md

1013 B

Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu.

Maelezo haya humaanisha: "Kristo kwa kupenda kwake mwenyewe aliutoa uhai wake kwa ajili yetu" au "Kristo kwa kupenda kwake alitufia sisi."

Mali za ulimwengu.

"Mali zinazomilikiwa kama vile pesa, chakula, au nguo."

Humuona ndugu yake mwenye uhitaji.

"Na humtambua muumini mwenzake anayehitaji msaada."

Na huufunga moyo wake wa huruma kwa ajili yake.

Maelezo haya humaanisha kwamba, "lakini hamwonei huruma." au lakini hapendi kumsaidia."

Upendo wa Mungu unakaaje ndani ya mtu huyo?

Yohana anatumia swali kuwafundisha wasikilizaji wake. Hii ingeweza kutafsiriwa kama usemi: "Upendo wa Mungu haumo ndani yake."

Watoto wangu wapendwa.

"Watoto au wapendwa waumini wenzi wangu."

Haya tusipende kwa maneno wala kwa mdomo.

Kifungu hiki, "kwa maneno" na "kwa mdomo" yote mawili yanalenga kile ambacho mtu anasema. " Usiseme tu ili mradi kwamba unawapenda watu."

Bali katika matendo na kweli

"Bali onesha kwamba kweli unawapenda watu kwa kuwasaidia."