sw_tn/mat/11/09.md

1.2 KiB

Sentesi unganishi:

Yesu aliendelea kuongea na umati kuhusu Yohana Mbatizaji.

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 10, Yesu anamnukuru nabii Malaki kuonyesha kuwa maisha na huduma ya Yohana imetimiza unabii.

Lakini mliondoka kuona nini--nabii?

Yesu anatumia swali ili kuwafikirisha watu juu ya Yohana mbatizaji kuwa ni mtu wa aina gani. "Lakinini kweli kwamba mlienda jajngwani kumuona nabii"

Lakini mlienda nje kuona nini--nabii? Ndiyo, nawaambia nyinyi.

Kiwakilishi cha wingi ''nyinyi'' inarejelea kwa katika hali zote.

ni zaidi ya nabii

Hii inaweza kutafsirika kama sentensi timilifu. "Siyo nabii wa kawaida" au ''siyo mtu wa kawaida'' au ''ni wa muhimu kuliko nabii wa kawaida''

huyu ndiye aliye andikiwa

Hii inaweza kutafsirika katik mfumo tendaji. "Hiki ndicho nabii Malaki aliandika zamamni za kale kuhusu Yohana mbatizaji"

namtuma mjumbe wangu

Kiwakilishi ''na'' na ''wangu'' kinamrejea Mungu. Malaki ananukuu ambacho Mungu alisema.

mbele ya uso wako

Kiwakilishi "wako" ni cha umoja kwa sababu Mungu alikuwa anasema juu ya Masihi katika nukuu.vPia "uso" inamaanisha nafsi timilifu, "mbele yako" au "kutangulia"

ataandaa njia yako

Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa mjumbe atawaandaa watu kupokea ujumbe wa Masihi.