sw_tn/1ti/01/03.md

983 B

Kauli Unganishi

Paulo anamtia moyo Timotheo kukataa matumizi mabaya ya sheria na atumie vizuri mafundisho kutoka kwa Mungu.

Kama nilivyokusihi wewe

"Kama nilivyokuhimiza wewe," au "Kama nilivyokuomba kwa bidii"

kaeni Efeso

"nisubirini mimi hapo katika mji wa Efeso"

mapokeo mengine

mafundisho mengine tofauti na yale tuliyofundisha sisi.

wala hawatasikiliza kwa makini

"Pia nataka ninyi muwaamuru wasisikilize kwa makini"

hadithi

zinaweza kuwa ni hadithi kuhusu mababu zao.

vizazi visivyo na mwisho

Paulo anatumia "isiyo na mwisho" kusisitiza kwamba vizazi ni vingi.

Hizi husababisha malumbano

"Hizi huwafanya watu kutokubaliana." Watu walijadili kuhusu hadithi na nasaba ambamo hakuna angeweza kujua ukweli wake.

badala ya kusaidia mpango wa Mungu, ambao ni kwa imani

Maana: 1) badala ya kutusaidia sisi kujua mpango wa Mungu wa kutuokoa, ambao tunajifunza kwa imani 2) badala ya kutusaidia sisi kufanya kazi ya Mungu, ambayo tunaifanya kwa imani