sw_tn/act/23/01.md

616 B

Sentensi unganishi

Paulo anasimama mbele ya wakuu wa makuhani na wajumbe wa baraza.

Ndugu zangu

Hii ina maana " Wayahudi."

Nimeishi mbele za Mungu na dhamiri njema mpaka leo

"Mimi najua kuwa hata leo nimefanya kila kitu Mungu alichotaka mimi kufanya"

Anania

Ni mtu tofauti na Anania anayetajwa sura ya 5:3

ukuta uliopakwa chokaa

Inamaanisha ukuta uliopakwa chokaa ili uonekane kuwa safi. Paulo anamwambia Anania kuwa anaonekana safi kama ukuta uliopakwa chokaa lakini ndani kumejaa uovu.

Umeketi kuhukumu ... kinyume cha sheria?

Paulo anatumia swali ili kumdhihirisha Anania kuwa ni mnafiki.