sw_tn/psa/060/010.md

670 B

Lakini wewe, Mungu, haujatukataa?

Mwandishi anatumia swali hili kueleza huzuni yake kuwa inaonekana kwamba Mungu amewakataa. "Lakini Mungu, inaonekana kama umetukataa." au "Mungu, inaonekana kama umetuacha"

Hauendi vitani na jeshi letu

Mwandishi anazungumzia Mungu kusaidia jeshi lao kana kwamba Mungu huwa anapigina pamoja nao. "huwa husaidii jeshi letu tunapoenda vitani"

haufai

"hauna maana"

tutashinda

"kuwa na ushindi"

atawakanyaga chini adui zetu

Mwandishi anazungumzia Mungu kusaidia jeshi lao kuwashinda adui zao kana kwamba Mungu alikuwa akiwakanyaga adui zao. "atatusaidia kuwakanyaga chini adui zetu" au "atatuwezesha kuwashinda adui zetu"