sw_tn/psa/059/006.md

1.0 KiB

Wanarudi jioni

Wanaorudi ni watenda maovu.

wanalia kama mbwa

Mwandishi anazungumzia vitishio vya adui zake kushambulia watu kana kwamba walikuwa ni mbwa wanaolia, kunguruma, au kubweka kwa watu. "wanatishia kushambulia watu"

kuuzunguka mji

"kuuzunguka mji kumshambulia yeyote watakayemkuta"

Tazama

Hapa neno "Tazama" linatumika kuvuta nadhari kwa kitu. "Sikia"

wanateuka kwa midomo yao

Kusema vitu viovu inazungumziwa kama kuteuka. Vitu hivi vibaya vinaweza kuwa ni matusi au vitisho. "wanasema vitu vibaya" au "wanapiga kelele kwa kusema vitu vibaya"

teuka

kutoa pumzi kwa nguvu kutoka mdomoni; kuruhusu hewa kutoka tumboni kupitia mdomoni kwa sauti kubwa ya kuudhi.

panga ziko kwenye midomo yao

Vitu vya ukatili ambavyo watu waovu walikuwa wakisema vinazungumziwa kana kwamba ni panga. "wanasema vitu vya ukatili vinavyosababisha watu taabu kama panga zinavyoangamiza watu"

Nani anatusikia?

Swali hili linatumika kuonesha kuwa waliamini kuwa Mungu hatawasikia na kuwaadhibu. "Hakuna mtu anayetusikia!" au "Mungu wenu hatusikii!"