sw_tn/psa/058/003.md

1.0 KiB

Waovu wanapotoka hata walipokuwa tumboni ... wanaenda pembeni tangu kuzaliwa

Hili ni wazo moja linaloelezwa kwa njia mbili tofauti.

wanapotoka

Kufanya vitu vibaya inazungumziwa kana kwamba watu wanatembea kwenye barabara, na wanageuka na kukosea njia. "wanafanya makosa"

Sumu yao ni kama sumu ya nyoka

Vitu viovu ambavyo watu wanasema vinazungumziwa kana kwamba ni sumu. "Maneno yao maovu yanasababisha shida kama sumu ya nyoka inavyowadhuru watu"

ni kama fira kiziwi anayezuia maskio yake

watu waovu wasiosikia ushauri au kukemewa wanazungumziwa kana kwamba ni nyoka ambazo haziitikii muziki wa mganga. "wanakataa kusikiliza kama fira kiziwi inayozuia maskio yake"

fira kiziwi anayezuia maskio yake

Fira asiyeitikia muziki wa mganga anazungumziwa kana kwamba inaweza kuweka kitu katika maskio yake ili kwamba isisikie. "fira asiye sikia"

fira

aina ya nyoka mwenye sumu

waganga

watu wanaocheza au kuimba muziki ili kumwongoza nyoka

haijalishi ujuzi wao ulivyo

"haijalishi ujuzi walionao waganga katika kumwongoza nyoka"