sw_tn/psa/046/010.md

689 B

Kuwa kimya na ujue kuwa mimi ni Mungu

Hapa, Mungu anaanza kuzungumza.

Kuwa kimya

Katika hali hii, maneno haya yanawezekana kuwa ni amri kwa mataifa kukomesha vita vyao. "Acheni kupigana"

ujue kuwa mimi ni Mungu

Hapa neno "kujua" inamaanisha kuelewa na kukiri kuwa Yahwe ndiye Mungu wa kweli.

Nitatukuzwa katika mataifa; nitatukuzwa duniani

Misemo hii miwili inamaana sawa na inasisitiza kuwa watu wa kila taifa duniani watamtukuza Mungu. "Watu katika kila taifa watanitukuza; watu duniani kote watanitukuza"

Yahwe wa majeshi yuko nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni sehemu ambayo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya ulinzi.