sw_tn/psa/081/006.md

732 B

Taarifa ya Jumla:

Hapa Mungu anaanza kuzungumza.

Nilitoa mzigo kutoka mabegani mwake

Hapa "mzigo kutoka mabegani mwake" inawakilisha kazi za kulazimishwa ambazo Waisraeli iliwalazimu kufanya kama watumwa Misri.

mikono yake iliwekwa huru na kushikilia kikapu

Hapa "kushikilia kikapu" inawakilisha kazi za kulazimishwa ambazo Waisraeli iliwalazimu kufanya kama watumwa Misri.

katika dhiki yako

"katika mateso yako makuu"

Nilikujibu kutoka katika wingu la giza la radi

Mungu alipokuja kwa Waisraeli, alificha ukamili wa uwepo wake na utukufu katika wingu lenye giza na la kutisha.

Nilikujaribu katika maji ya Meriba

Mungu aliwajaribu wana wa Israeli kuona kama watamtumaini kuwapa maji katika jangwa la Meriba.