sw_tn/act/17/01.md

1.0 KiB

Sentensi unganishi

Habari kuhusu Paulo na Sila inaendelea pamoja na Timotheo katika safari yao ya kimisionari. Walifika Thesalonike na Luka hakuwa pamoja nao.

Taarifa za jumla

Ni habari kuhusu Paulo na Sila pamoja na Wayahudi katika Sinagogi huko Thesolanike

Sasa

Ni neno linalogawanya habari iliyokuwa ikiendelea kwa kutaja jambo jingine. Luka anaanza kuelezea sehemu mpya ya tukio.

walipopita

"Kusafiri kupitia"

miji ya Amfipoli na Apolonia

Hii ni miji ya mwambao huko Makedonia

walifika mjini

Neno linaloonyesha kuwa walisafiri hadi kufika mjini.

kama ilivyokuwa kawaida

" kama ilivyokuwa kawaida yake" au "Kama alivyofanya siku zote". Mara kwa mara Paulo alikuwa na ya kuingia kwenye Sinagogi siku ya sabato mahali wayahudi walikusanyuka.

kwa sabato tatu

"katika kila siku ya sabato kwa majuma matatu".

alihojiana nao kutoka kwenye maandiko

"alijadiliana na Wayahudi wa Sinagogi" au walijadili na Wayahudi wa Sinagogi"

alihojiana nao

"aliwapa sababu" au "kuhojiana pamoja nao" au "kuzungumza pamoja nao".