sw_tn/act/13/11.md

826 B

Sentensi unganishi

Paulo anamalizia majadiliano na Elima.

mkono wa Bwana upo juu yako

Neno "mkono" unawakilisha nguvu za Mungu na neno "juu yako" linamaanisha adhabu . "Mungu atakuadhibu"

utakuwa kipofu.

Hii inaweza kutafsiriwa kuwa; "Mungu atakufanya kipofu"

Hautaliona Jua

Elima atakuwa kipofu kabisa kwamba hataweza kuliona jua.

kwa muda

"Kwa kipindi fulani" au "Mpaka muda wa Mungu aliouamru"

mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas

"Macho ya Elima yakapata ukungu na giza" au "Elima uoni ulikuwa hafifu na kisha hakuweza kuona kabisa"

alianza kuzunguka pale

"Elima alianza kutangatanga"

Liwali

Huyu alikuwa ni mtumishi wa serikali katika jimbo la Rumi.

Aliamini

"Alimwamini Yesu"

alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.

"Mafundisho kuhusu Bwana Yesu yalimshangaza mno"