sw_tn/act/10/01.md

745 B

Sentensi unganishi

Huu ni mwanzo wa sehemu juu ya habari inayohusu Kornelio.

Maelezo ya jumla

Mistari hii inatupa mrejesho wa taarifa kuhusu yeye.

Kulikuwa na mtu fulani

Hii ilikuwa ni njia ya kutambulisha mtu mwingine katika habari.

jina lake aliitwa Cornelio, alikuwa mkuu wa kikosi cha Kiitalia

"jina lake aliitwa Kornelio. alikuwa ni mtu mwenye cheo wa maaskari 100 kutoka Italia katika sehemu ya jeshi la Rumi"

Alikuwa mcha Mungu na alimwabudu Mungu

"Aliamini katika Mungu na alitaka kumtii Mungu na kumwabudu Mungu katika maisha yake"

na nyumba yake yote

"na watu wote wengine wa nyumbani kwake ambao pengine walikuwa wa mataifa walimcha Mungu"

aliomba kwa Mungu siku zote.

Alikuwa akimwomba Mungu wakati wote.