sw_tn/act/08/intro.md

1.3 KiB

Matendo 08 Maelezo ya jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zimeweka kila mstari wa ushairi mbele ya kulia kuliko maandishi mengine ili kurahisisha kusoma. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la Kale 8:32-33

Sentensi ya Kwanza ya mstari wa 1 inaishia na maelezo ya matukio ya sura ya 7: Luka anaanza sehemu mpya ya historia yake na maneno "Hapo ikaanza".

Dhana maalum katika sura hii.

upokea Roho Mtakatifu

Katika sura hii, Luka anawazungumzia kwa mara ya kwanza juu ya watu wanaopokea Roho Mtakatifu (Matendo 8:15-19).Roho Mtakatifu alikuwa mbele amewawezesha waumini kunena kwa lugha, kuwaponya wagonjwa na kuishi kama jumuia na alikuwa amemjaza Stefano pia. Lakini wakati Wayahudi walipoanza kuwafunga waumini katika gereza waumini walioweza kutoroka Yerusalemu walitoroka na walipokuwa wakiondoka waliwahubiria watu kumhusu Yesu. Wakati watu waliosikia ujumbe kuhusu Yesu walipokea Roho Mtakatifu, viongozi wa kanisa walijua kwamba watu hao walikuwa waumini wa ukweli.

Ilitangazwa

Sura hii inazungumzia waumini wakitangaza neno, habari njema na kumtangaza Yesu kwamba ndiye Kristu kuliko sura zingine za kitabo cha Matendo. Neno "tangaza" ni tafsiri ya neno la Kigiriki linalomaanisha kusema habari njema kuhusu jambo ama kitu.

<< | >>