sw_tn/act/01/01.md

758 B

Sentensi unganishi.

Luka anaelezea ni kwasababu gani anamwandikia Theofilo

Kitabu cha zamani nilikiandika

Kitabu cha zamani ni Injili ya Luka.

Theofilo

Luka aliandika kitabu hiki kwa mtu anayeitwa Theofilo. Baadhi ya watafsiri hufuata mfumo wa tamaduni zao za kuelezea barua na huandika "Mpendwa Theofilo" mwanzoni mwa sentensi. Theofilo humaanisha "rafiki wa Mungu.

Mpaka siku alipopokelewa juu

Hii inarejesha kwenye kupaa kwa Yesu mbinguni

Amri kupitia kwa Roho Mtakatifu

Roho Mtakatifu alimwongoza Yesu kuwaelekeza mitume wake juu ya vitu fulani.

Baada ya kuteswa kwake

Hii inahusu mateso ya Yesu na kifo chake msalabani.

Alijidhihirisha Yeye mwenyewe akiwa hai

Yesu alionekana kwa mitume wake na kwa wanafunzi wengi wengine.