sw_tn/2pe/01/intro.md

1.3 KiB

2 Petero 01 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Kumjua Mungu

Kumjua Mungu inamaanisha kumilikiwa naye ama kuwa na uhusiano naye. Hapa "ujuzi" ni zaidi ya kumjua Mungu na akili. Ni ujuzu unaomfanya Mungu kumuokoa mtu na kumpa neema na amani. (Tazama: rc://en/tw/dict/bible/other/know)

Kuishi maisha ya ya kumcha Mungu

Petero anafundisha kwamba Mungu amewapa waumini yote wanayohitaji kuishi maisha ya kumcha Mungu. Kwa hivyo waumini wafanye kila waezalo kumtii Mungu zaidi. Waumini wakiendelea kufanya hivyo watakuwa imara na wenye manufaa kupitia uhusiano wao na Yesu. Lakini waumini wasipoendelea kuishi maisha ya kumcha Mungu, watakuwa ni kama wamesahau walichofanyiwa na Mungu kupitia kwa Kristo kuwaokoa. (Tazama: rc://en/tw/dict/bible/kt/godly and rc://en/tw/dict/bible/kt/save)

Maswala mengine ya utata ya kutafsiri katika sura hii

Ukweli wa Maandiko

Petero anafundisha kwamba unabii wa maandiko haukutolewa na binadamu. Roho Mtakatifu alifunua ujumbe wa Mungu kwa watu waliouandika kwa kitabu. Petero pia na Mitume wengine hawakubuni hadithi walizowapa watu kuhusu Yesu. Walishuhudia chenye Yesu alifanya na wakamsikia Mungu akimwita Yesu mwanawe.

| >>