sw_tn/2co/06/intro.md

1.8 KiB

2 Wakorintho 06 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa mistari 2 na 16-18, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Watumishi

Paulo anawakilisha Wakristo kama watumishi wa Mungu. Mungu anawaita Wakristo kumtumikia katika hali zote. Paulo anaelezea baadhi ya hali ngumu ambako yeye na wenzake walimtumikia Mungu.

Mfano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maneno ya tofauti

Paulo anatumia jozi nne za utofauti: haki dhidi ya uasi, mwanga dhidi ya giza, Kristo dhidi ya Shetani, na hekalu la Mungu dhidi ya sanamu. Tofauti hizi zinaonyesha tofauti kati ya Wakristo na wasio Wakristo. (See: rc://en/tw/dict/bible/kt/righteous]] and rc://en/tw/dict/bible/other/light and [[rc://en/tw/dict/bible/other/darkness)

Mwanga na giza

Biblia mara nyingi inazungumzia watu wasio na haki, watu ambao hawampendezi Mungu, kama kwamba walikuwa wakizunguka gizani. Inazungumza juu ya mwanga ni kama inawawezesha watu wenye dhambi kuwa waadilifu, na kuelewa kile wanachokosea na kuanza kumtii Mungu. (See: rc://en/tw/dict/bible/kt/righteous)

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali ya uhuishaji mfululizo kwa kufundisha wasomaji wake. Maswali haya yote yana maana sawa sawa: Wakristo hawapaswi kushirikiana na wale wanaoishi katika dhambi. Paulo anarudia katika maswali haya kwa msisitizo. (See: rc://en/ta/man/translate/figs-rquestion]] and [[rc://en/tw/dict/bible/kt/sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Sisi

Labda Paulo anatumia neno "sisi" kuwakilisha Timotheo na yeye mwenyewe. Au labda anawajumuisha watu wengine pia.

<< | >>