sw_tn/1ti/05/01.md

755 B

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kumuasa Timotheo awajali wanaume, wanamke, wajane na wanawake wazee ndani ya kanisa.

Taarifa ya jumla:

Paulo alikua anatoa maagizo haya kwa mtu mmoja, Timotheo.

Usimkemee mwanaume mzee.

"Usiongee kwa ukali kwa mzee wa kiume"

Ila msihi kama baba

"Ila mtie moyo kama uongeavyo na baba yako," kwa adabu.

Msihi kijana wa kiume kama ndugu

"Mtie moyo vijana wa kiume kama ndugu zako" au "wafundishe vijana wakiume kama ambavyo ungefundisha ndugu zako," kwa amani.

Wanawake vijana kama dada

"wasihi wanawake vijana kama ambavyo unge wasihi dada zako" au "wafundishe wanawake vijana kama ambavyo ungewafundisha dada zako,"

Kwa usafi wote

"kwa mawazo safi na matendo" au "katika hali ya utakatifu"