sw_tn/1jn/02/01.md

1.2 KiB

Sentensi Unganishi

Yohana anaendelea kuandika juu ya ushirika na anaonyesha kwamba inawezekana kwa sababu Yesu yuko kati ya waaminio na Baba.

Maelezo ya Jumla

Hapa maneno "tunaye' na "zetu" humaanisha Yohana na waaminio wote. Neno "Yeye" na "zake" yaweza kumaanisha Mungu Baba au Yesu.

Watoto

Yohana alikuwa mzee na kiongozi wao. Alitumia maelezo haya kuonyesha pendo lake kwao. : "Watoto wangu wapendwa katika Kristo" au "Ninyi mliowapendwa kwangu kama watoto wangu mwanyewe"

ninawaandikia mambo haya

"Ninaandika barua hii"

Lakini kama mmoja wenu akitenda dhambi

"Lakini mmoja wenu anapotenda dhambi." Hili ni jambo ambalo inawezekana likatokea"

tunaye wakili aliye pamoja na Baba,

Neno "wakili" hapa humaanisha Yesu. : "mtu anayezungumza kwa Mungu Baba na kumsihi yeye apate kutusamehe sisi"

eye ni upatanisho kwa dhambi zetu, na siyo kwa dhambi zetu

"Aliyatoa dhabifu maisha yake mwenyewe kwa ajili yetu, na kwa sababu ya hilo Mungu husamehe dhambi zetu"

Kwa hili twajua kwamba , kama tukizishika amri zake.

"Kama tunafanya anayotuambia kufanya, kisha tutakua na uhakika kwamba tunao uhusiano na yeye"

tunamjua yeye

"tunao uhusiano na yeye"