sw_tn/zec/01/16.md

785 B

Nimeirudia Yerusalemu kwa rehema nyingi

Kurudi Yerusalemu inamaanisha kuchukua tena jukumu la kuwaudumia watu wa Israeli kama mfalme kurudi kuwaongoza watu kutoka katika shida.

Nyumba yangu itajengwa ndani yake

"Hii inamaanisha kujengwa tena kwa hekalu katika Yerusalem"

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe." Na kifungu hiki kimetumika mara kwa mara katika kitabu hiki.

Kipimo kitanyoshwa juu ya Yerusalemu

"Yerusalemu itakaguliwa kabla ya kujengwa"

Miji yangu kwa mara nyingine itajawa na uzuri

Yahwe anamaanisha mambo mema atakayoyafanya kwa ajili ya watu wake Israeli kama ambavyo kimiminika kinavyoweza kujaa katika miji na kufurika.

Yahwe ataifariji tena Sayuni

"Yahwe atawatia moyo watu wa Israeli"