sw_tn/rev/17/01.md

675 B

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza sehemu ya maono yake kuhusu kahaba mkuu.

hukumu ya kahaba mkuu akaaye juu ya maji mengi

Nomino "hukumu" linaweza kuelezwa na kitenzi "kuhukumu". "jinsi gani Mungu atamhukumu kahaba mkuu aliyeketi juu ya maji mengi"

kahaba mkuu

"kahaba ambaye kila mmoja anamfahamu." Anawakilisha mji flani wenye uovu.

juu ya maji mengi

"juu ya mito mingi"

na juu ya mvinyo wa uasherati wake wakaao duniani wameleweshwa

Divai inawakilisha uasherati. "Watu wa duniani walilewa kwa kunywa divai yake, ambayo ni, walikuwa washerati"

uasherati wake

Hii inaweza kuwa na maana mbili: uasherati miongoni mwa watu na pia kuabudu miungu.