sw_tn/rev/03/03.md

762 B

yale uliyoyapokea na kusikia

Hii humaanisha neno la Mungu ambalo waliamini. "neno la Mungu mlilosikia na ukweli mlioamini"

usipoamka

Kuwa makina na hatari huzungumziwa kama kuamka. "Kuwa makini" au "Kuwa mwangalifu."

nitakuja kama mwivi

Yesu atakuja wakati watu hawatarajii kama vile mwizi ajavyo asipotarajiwa.

majina machache ya watu

Hii humaanisha watu wenyewe. "watu wachache"

hawakuchafua nguo zao

Yesu anazungumzia dhambi katika maisha ya mtu kama vile ni nguo chafu. "hawajafanya maisha yao yawe yenye dhambi kama nguo chafu"

Watatembea pamoja nami

Watu kawaida walizungumzia kuishi kama "kutembea."

wamevaa nguo nyeupe

Nguo nyeupe huashiria maisha masafi bila dhambi. "na watavikwa nguo nyeupe ambayo inaonesha waso ni wasafi"