sw_tn/psa/083/013.md

611 B

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anatumia tashbihi kuelezea uharibifu kamili wa Mungu kwa adui wa Israeli.

wafanya kuwa kama mavumbi yanayozunguka, kama makapi mbele ya upepo

Kauli zote mbili zinazungumzia Mungu kuangamiza adui zake kana kwamba alikuwa upepo mkali unaowapuliza kwa urahisi.

kama moto unaochoma msitu, na moto unaoweka milima katika moto

Kauli zote mbili zinazungumzia adhabu ya Mungu kana kwamba ni moto, na adui wa Mungu ni vitu vinavyoungua katika moto.

Wafukuze kwa upepo wako wenye nguvu, na watishe kwa dhoruba yako

Kauli zote mbili zinamwomba Mungu kuangamiza adui kwa dhoruba.