sw_tn/psa/078/056.md

612 B

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

walipingana na kukaidi

Maneno haya yana maana ya kukaribiana. Mwandishi anayatumia yote kusisitiza kuwa Waisraeli hawakuamini kuwa Mungu atawap mahitaji au kuadhibu maovu kama alivyosema atafanya.

walipingana

Walitaka Mungu kuthibitisha kuwa anaweza kufanya kama alivyosema kabla hajamwamini.

kukaidi

"kataa kutii"

Hawakuwa waaminifu na kutenda kwa uongo

Maneno haya yana maana ya kukaribiana. Mwandishi anayatumia yote mawili kusisitiza kuwa Waisraeli hawakumfanyia Mungu walichosema watafanya.