sw_tn/psa/044/012.md

963 B

Unawauza watu wako bure

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwaruhusu adui wa Israeli kuwashinda kana kwamba alikuwa akiwauza watu wa Israeli kwa adui zao lakini hahitaji malipo kutoka kwa adui zao.

Unatufanya kuwa lawama kwa jirani zetu, kudhihakiwa na kukejeliwa na wale waliotuzunguka

Misemo hii miwili ina usambamba ikisisitiza jinsi watu wanaoishi miongoni mwao wanavyowakejeli.

Unatufanya kuwa lawama kwa jirani zetu

"Unatufanya kuwa kitu ambacho jirani zetu wanakemea"

kudhihakiwa na kukejeliwa na wale waliotuzunguka

"wale waliotuzunguka wanatudhihaki na kutukejeli"

fedheha miongoni ... kutikisa kichwa

Misemo hii miwili ina usambamba ikisisitiza jinsi watu wanavyowakejeli kwa nguvu.

Umetufanya fedheha miongoni mwa mataifa

Unayafanya mataifa yaliyo tuzunguka kutufedhehesha"

kutikisa kichwa miongoni mwa watu

"jambo ambalo watu hutikisa vichwa"

kutikisa kichwa

Hiki ni kitendeo ambacho watu walitumia kuonesha dharau wengine.