sw_tn/psa/035/004.md

1.0 KiB

Na wale wanaotafuta maisha yangu waaibike na kunyimwa heshima

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe awaaibishe na kuwanyima heshima wale wanaotafuta maisha yangu"

Na

"Natamani kwamba"

wanaotafuta maisha yangu

Hapa "maisha yangu" inamaana wanatamani kumuua mwandishi. "wanaojaribu kuniua"

Na wale wanaopanga kunidhuru wageuzwe na washangazwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe awageuze na kuwashangaza wale wanaopanga kunidhuru"

wageuzwe

"wageuzwe" ni sitiari ya kushindwa kutimiza lengo lao. "kushindwa kufanikiwa"

washangazwe

"wachanganyikiwe" au "kuwafadhaisha"

kama makapi mbele ya upepo

Adui wa mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni nyasi ambayo inapulizwa kwa urahisi. "kupulizwa na upepo kama makapi"

njia yao

Hapa "njia yao" inamaanisha maisha yao. "maisha yao"

giza na utelezi

Hii inamaanisha njia iliyojificha na hatari. "imejificha na imejaa hatari"

anawafukuza

Hii inamaanisha malaika wa Yahwe kuwa kinyume na adui wa mwandishi. "anaenda kinyume nao" au "anawapinga"